Serikali ya Kenya imetangaza
hali ya ukame iliyoko sasa iliyoathiri kaunti 23 zenye ukame na baadhi
ya maeneo mengine kuwa ni janga la taifa.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amewataka wadau wote kuiunga mkono
serikali kwa kuongeza miradi ya kukabiliana na ukame ambao umewaacha
watu zaidi ya milioni 2 wakihitaji msaada wa dharura wa chakula. Amesema
kuungwa mkono na wedau hao kutasaidia juhudi za serikali katika
kudhibiti madhara ya ukame.
Rais Kenyatta pia ametoa wito kwa wadau wa ndani na nje ya nchi
kuungana na kusaidia juhudi za serikali kudhibiti hali hiyo ambayo sio
tu inaathiri binadamu na wanyama, lakini pia inaathiri wanyamapori.
Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa FAO limeonya
kuwa Kenya inakabiliwa na hali mbaya ya ukame unaosababisha uhaba wa
chakula.
Kenya yatangaza ukame kuwa janga la taifa
Reviewed by Mipiko
on
9:36 AM
Rating: 5