Breaking News

CHICHARITO AJIUNGA NA KLABU YA WEST HAM

Mshambulizi wa zamani wa Klabu ya Manchester United Javier Hernandez hatimaye amesajiliwa na West Ham kwa pauni milioni 16.

Raia huyo wa Mexico alikubali mkataba wa kumtoa kutoka Ujerumani na klabu ya Bayer Leverkusen na anasubiri uchunguzi wa kimatibabu tu kabla ya kukamilisha uamisho huo.

Hernandez ambaye anafahamika sana kama Chicharito amekuwa mchezaji wa Mexico aliyefunga mabao mengi zaidi kwa historia baada ya kutinga bao lake la 47 la kitaifa mwezi mei.