Kamanda wa Polisi mkoa wa MOROGORO, URLICH MATEI
Jeshi la polisi mkoani MOROGORO linamshikilia mtu mmoja
SHABANI MZIBA mkazi wa mji mpya manispaa ya MOROGORO kwa kosa la
kujifanya Afisa wa Jeshi hilo mwenye cheo cha ASP.
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro ULRCHI MATEI amesema mnamo Novemba
30 mwaka huu, majira ya saa 11 jioni maeneo ya KINGOLWIRA manispaa ya
MOROGORO mtuhumiwa alijifanya yeye ni afisa wa jeshi hilo na
kughushi mhuri wa kituo cha polisi kati MOROGORO kinyume cha sheria.
Mtuhumiwa SHABANI MZIBA anadaiwa kuwa alighushi muhuri wa kituo cha
polisi cha kati morogoro na kumwandikia barua MAZAO NGALE mkazi wa Mkono
wa Mara akimtaka waonane kujadili kesi inayomkabili ya kuoa mtoto
mdogo.
Katika tukio lingine jeshi la polisi mkoani Morogoro limemfikisha
mahakamani mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la KAJUNA RWEYEMAMU mkazi
wa Mbagala jijini Dar es Salaam na kisha kuhukumiwa kifungo cha mwaka
mmoja jela kwa kosa lawizi wa shilingi milioni 3.