Uwanja wa Ndege wa Madeira Wapewa Jina la Cristiano Ronaldo.
Ronaldo ambaye alizaliwa katika mji mkuu wa Madeira, Funchal na baadaye akachezea Sporting Lisbon na Manchester United.
Uwanja wa ndege wa Madeira sasa umepewa jina la Cristiano Ronaldo.
Baadhi ya wanasiasa wa eneo hilo wamepinga uamuzi wa kubadilisha jina la uwanja wa ndege wa Madeira kuwa Uwanja wa Ndege wa Cristiano Ronaldo.
“Wakati mwingine, shukrani za taifa huwa hazidumu sana, lakini Madeira haitasahau,” Miguel Albuquerque, rais wa serikali ya Madeira alitangaza, hatua ya kubadilisha jina la uwanja huo ilipotangazwa.