Mfanyabiashara Yusuf Manji Jumapili ya jana alionekana
akitolewa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi na kupandishwa kwenye gari la
wagonjwa ambalo lilipita Barabara ya Sokoine kuelekea Posta Mpya.
Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Manji alipanda gari hilo la
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) lakini
hawakufahamu mara moja alikoelekea.
Manji alikuwa amevaa fulana, suruali na viatu vya wazi vyote vya rangi nyeusi
Mwenyekiti
huyo wa Yanga anashikiliwa na jeshi hilo kwajili ya mahojiano kuhusu
tuhuma zinazomkabili za kujihusisha na biashara ya Madawa ya kulevya.
Picha: Manji aonekana akitolewa polisi na gari la wagonjwa
Reviewed by Mipiko
on
7:58 AM
Rating: 5