Breaking News

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa amtaka rais mpya wa Somalia aunde serikali shirikishi haraka iwezekanavyo


Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amempongeza waziri mkuu wa zamani wa serikali ya mpito ya Somalia Bw. Mohammed Abdullahi Mohammed kwa kuchaguliwa kuwa rais wa Somalia na kumtaka aunde serikali shirikishi haraka iwezekanavyo.

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Katibu mkuu huyo imesema, Bw. Guterres amesema serikali mpya na wajumbe wa shirikisho wanapaswa kukabiliana na masuala ya dharura ya nchi hiyo kwa pamoja, ikiwemo kutunga katiba na kuunda jeshi la ulinzi la taifa.

Amesema hivi sasa Somalia inakabiliwa na ukosefu wa chakula uliotokana na ukame, na Umoja wa Mataifa unapenda kutoa msaada kwa Somalia.