Serikali za Tanzania na Zambia zimeahidi kuimarisha utendaji kazi wa
reli ya TAZARA na mradi wa bomba la mafuta la TAZAMA yanayoendeshwa
kwa ushirikiano wa baina ya nchi hizo.
Akizungumza leo, Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais wa Zambia Edgar
Lungu amesema kuwa Tanzania na Zambia zitaendelea kushirikiana
kuiboresha reli hiyo ili iweze kufanya kazi kwa ufanisi.
Kwa upande wake Rais John Pombe Magufuli amesema Reli ya TAZARA na
bomba la Mafuta la TAZAMA zinakabiliwa na changamoto za mtaji na uongozi
na hivyo kufanya reli hiyo kuwa na uwezo wa kusafirisha mizigo tani
128,000 tu, ambapo ilipoanzishwa mwaka 1976 ilikua na uwezo wa kubeba
mizigo tani 500,000.
Ili kutatua changamoto hizo Rais Magufuli amesema kuwa “tumekubaliana
kubadilisha menejimenti ya TAZARA, kubadilisha sheria ili kuwezesha
menejimenti hiyo kuongozwa na mtu mwenye uwezo ambaye si lazima awe
anatoka Tanzania au Zambia”.
“Nia ya Serikali hizi ni kuongoza reli hiyo kibiashara kwa maslahi na maendeleo ya nchi zote mbili” alisema Rais Magufuli.
Kwa mujibu wa Rais Magufuli malengo ya Serikali zote mbili ni kupunguza
ucheleweshaji mizigo kufika nchini Zambia, ambapo wamekusudia
kupunguza vituo vya kukagua magari ya mizigo hadi kufikia vinne.
Sambamba na hayo Serikali hizi mbili zimesaini makubaliano ya kuwepo
kwa mashaurinao ya kidiplomasia, pamoja na kuahidi kuendeleza
ushirikiano wa kihistoria baina ya nchi hizi mbili.
ZIARA YA RAIS WA ZAMBIA YALETA NEEMA NCHINI....TANZANIA NA ZAMBIA ZAKUBALIANA KUIMARISHA RELI YA TAZARA
Reviewed by Mipiko
on
6:00 PM
Rating: 5