Breaking News

Afrika haipaswi kutenganisha sekta za uchumi, jamii na mazingira katika kujiendeleza






Naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Carlos Lopes amesema, Afrika haipaswi kutenganisha sekta za uchumi, jamii na mazingira katika njia ya kujiendeleza.

Lopes ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa Kamati ya Uchumi wa Afrika kwenye Umoja wa Mataifa amesema hayo huko Lome ambako anashiriki mkutano wa Umoja wa Afrika kuhusu mambo ya usalama wa bahari na maendeleo. Amesema, serikali za nchi za Afrika, jumuia za kiraia na wenzi wa ushirikiano wanapaswa kusukuma mbele maendeleo ya uchumi, jamii na mazingira ya Afrika kwa wakati mmoja, na Umoja wa Mataifa unapaswa kutoa msaada wa rasilamili.

Ameongeza kuwa uchumi wa Afrika upo kwenye mchakato wa kubadilika, na kwamba sehemu kubwa ya ongezeko la uchumi huo inatokana na ongezeko la soko la ndani, lakini ongezeko hilo halichangii mapato ya serikali kutokana na kodi ya kiwango cha chini.

Bw. Lopes pia amezihimiza nchi za Afrika kuyaongezea kodi makampuni makubwa ili kukabiliana na upungufu wa misaada.