NAIBU WAZIRI WA ELIMU MHANDISI STELLA MANYANYA ALIVYO FUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO KUMBUKIZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE
Naibu
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mhandisi
Stella Manyanya (kulia), akihutubia wakati alipokuwa akifungua kongamano
la maadhimisho ya kumbukizi ya Mwalimu Julius Nyerere lililofanyika
Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni Dar es Salaam jana.
Naibu
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mhandisi
Stella Manyanya (katikati), akisalimiana na wafanyakazi wa Chuo cha
Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere alipokuwa amewasili kwenye kongamano la
maadhimisho ya kumbukizi ya Mwalimu Julius Nyerere lililofanyika chuoni
hapo Dar es Salaam jana. Kushoto ni mkuu wa chuo hicho, Profesa Shadrack
Mwakalila. Manyanya alikuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo.
Taswira ya ukumbi katika kongamano hilo.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation, Joseph Butiku akitoa mada kwenye kongamano hilo.
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Mwenyekiti wa kongamano hilo, Spika wa Bunge mstaafu, Anna Makinda akizungumza kwenye kongamano hilo.
wadau mbalimbali wakiwa kwenye kongamano hilo.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Philipo Mangula akitoa mada kwenye kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Mkuu
wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Profesa Shadrack Mwakalila,
akizungumza kwenye kongamano hilo. Kongamano hilo liliandaliwa na chuo
hicho.
Waalikwa wakisikiliza wakati mada zikiendelea kutolewa.


