China yaimarisha Ushirikiano baina yake na Afrika
Kongamano la pili la uwekezaji
barani Afrika limemalizika jana jijini Guangzhou, China ambapo kampuni
za China na Afrika zimesaini makubaliano ya uwekezaji yenye thamani ya
zaidi ya dola za kimarekani bilioni 25.
Katika miaka ya hivi karibuni ushirikiano kati ya China na Afrika
umeelekea kwenye uwekezaji na viwanda vya kuongeza thamani ya bidhaa
kutoka biashara ya moja kwa moja. Aidha, kampuni za China zinashiriki
zaidi kwenye kuendesha miundombinu na maeneo maalum ya viwanda barani
Afrika na huduma za fedha, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo zilifanya
kazi za ukandarasi wa miradi ya ujenzi.
Miradi iliyosainiwa kwenye mkutano huo ni pamoja na uzalishaji wa
umeme kwa kutumia muhogo na mua, na uendeshaji wa bandari ya Mombasa.