Breaking News

China yapeleka madaktari kutoa misaada katika eneo liliokumbwa na tetemeko la ardhi nchini Tanzania.

China imepeleka madaktari watano mkoani Kagera, Tanzania, kusaidia kutoa matibabu kwa watu walioathiriwa na tetemeko la ardhi lililotokea jumamosi iliyopita na kusababisha vifo vya watu 17 na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa.

Taarifa iliyotolewa na Ubalozi wa China nchini Tanzania imesema, madaktari hao ni pamoja na madaktari wa magonjwa ya wanawake, watoto, upasuaji, na wa magonjwa ya kawaida.

Ujumbe wa mabalozi kutoka nchi mbalimbali nchini Tanzania pamoja na jamii ya wafanyabiashara ulitoa mchango wa dola za kimarekani laki 7 na vifaa vingine vya kuwasaidia watu waliokumbwa na maafa hayo.