YALIYOJIRI KATIKA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO,MHE.DKT. PHILIP I. MPANGO (MB),ALIPOWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA UCHUMI 2016 NA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA KWA MWAKA 2017/18
#Kasi ya ukuaji wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2016,ilikuwa asilimia 3.1 ikilinganishwa na asilimia 3.2 mwaka 2015-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Mfumuko wa bei duniani uliongezeka kufikia wastani wa asilimia 2.9 mwaka 2016 ikilinganishwa na asilimia 2.8 mwaka 2015-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Pato la Taifa lilikuwa kwa wastani wa asilimia 7.0 kwa mwaka 2016-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Pato la Taifa kwa mwaka 2016 lilifikia Shilingi milioni 103,744,606-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Wastani wa pato la kila mtu limefikia Shilingi 2,131,299 ikilinganishwa na wastani wa Shilingi 1,918,897 mwaka 2015-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Mwaka 2016 mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 5.6 mwaka 2015-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Tanzania ni nchi ya tano kwa idadi ya watu Barani Afrika-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi wa Reli ya Kati kutoka Dar es Salaam-Morogoro(Km 205)-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali imenunua ndege mbili zenye uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja-Dr. Philip Mpango
#Serikali imesaini mkataba wa makubaliano ya awali ya ujenzi wa Bomba la mafuta kutoka Hoima Uganda-Bandari ya Tanga-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Ujenzi wa meli mbili za mizigo ziwa Nyasa umekamilika-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Shilingi Billioni 2 zimewekwa kwa ajili ya uanzishwaji wa Shamba la Miwa na Kiwanda cha Sukari Mkulanzi-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Mkoa wa Pwani una jumla ya miradi mipya ya viwanda 82-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Mapato ya kodi kufikia asilimia 14.2 ya Pato la Taifa mwaka 2017/18-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kufufua kiwanda cha sukari katika Gereza la Mbigiri Dakawa-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kufufua kiwanda cha kutengeneza viatu katika Gereza la Karanga Moshi-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kufufua kiwanda cha nguo cha Urafiki-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kufufua kiwanda cha Morogoro Canvas Mill-Mhe.Dr. Philip Mpango
#Serikali kufufua kiwanda cha chai cha Mponde kilichopo Lushoto,Tanga-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kufufua kiwanda cha Kilimanjaro Machine Tools-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kufufua kiwanda cha Kubangua Korosho cha Tandahimba na Newala-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kuanzisha viwanda vipya vya Dawa,vifaa vya hospitali na gesi ya oksijeni na kiwanda cha kusindika zabibu Chinangali Dodoma-Mhe. Dr. Philip Mpango
#Serikali kuanzisha kiwanda cha kuzalisha wanga kutokana na zao la muhogo na viazi vitamu huko Lindi-Mhe. Dr. Philip Mpango


