Breaking News

SIMBA SC WADAI KUONEWA SANA KWENYE SOKA...WAJIPANGA KWENDA FIFA ILI HAKI IPATIKANE.


 
Responsive image

Timu ya Simba ya jijini Dar es salaam  imesema tayari imewasiliana na shirikisho la kimataifa la vyama vya mpira wa miguu duniani FIFA kuhusu malalamiko ya kutokutendewa haki katika mfumo mzima wa uendeshaji wa mpira wa miguu hapa nchini.

Makamu wa rais wa Simba, Geofrey Nyange maarufu kama Kaburu amesema baada ya kupokea barua ya kunyang'anywa alama tatu kwa sasa wanajiandaa rasmi kwenda FIFA kwaajili ya kuwasilisha malalamiko yao na wanaamini kupitia FIFA haki yao itapatikana.

Aidha Kaburu amewataka wanachama wa Simba kuwa watulivu kwani timu hiyo ina fedha za kutosha kugharamia kesi hiyo pindi itakapofikishwa rasmi FIFA.