Breaking News

SERIKALI YAAHIDI NEEMA TAASISI ZA KIDINI.

Responsive image
Askofu wa Jimbo Katoliki Moshi, Mhashamu Isack Amani akimuombea rais Dkt. John Magufuliibada wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa la Kiaskofu Kristo Mfalme Jimbo Katoliki Moshi
 
Rais Dkt. John Magufuli amesema atamwagiza Waziri wa Fedha na Mipango kuangalia namna ya kuziondolea kodi Taasisi za kidini katika vifaa vinavyoingizwa nchini kwa ajili ya kutolea huduma kwenye Taasisi mbalimbali zinazosimamiwa na makanisa.
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akishiriki ibada ya Jumapili katika Kanisa la Kiaskofu Kristo Mfalme Jimbo Katoliki Moshi pamoja na Kanisa la KKKT Usharika wa Moshi Mjini.
Katika Kanisa la KKKT Usharika wa Moshi Mjini , Askofu Mkuu wa KKKT Dkt.  Fredrick Shoo amemuomba Rais  John Magufuli kuwapunguzia kodi katika vifaa wanavyoagiza kwa ajili ya kutolea huduma kwenye Taasisi za dini.
Akiwa katika Kanisa la Kiaskofu la Kristo Mfalme Jimbo Katoliki Moshi, Rais Magufuli amesisitiza suala la amani na upendo. 
Kwa upande wake Askofu wa Jimbo Katoliki Moshi,  Mhashamu Isack Amani ametoa wito kwa wananchi kuunga mkono juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya uhalifu. 
Rais Magufuli ametoa mifuko mia mbili ya saruji na shilingi milioni mbili kwa kwaya katika makanisa hayo.