Breaking News

RAMA DEE AFUNGUKA JINSI ANAVYOMKUBALI RAIS MAGUFULI.



Msanii Rama Madee amesema yeye ni kati ya watu ambao wanamkubali Rais Magufuli kutokana na uthubutu wa kiongozi huyo katika kufanya mambo yake ambayo kama kweli atayasimamia na kuyafanyia kazi kiuhalisia basi yatasaidia nchi kupiga hatua zaidi.

Rama Dee amesema hayo katika kipindi cha KIKAANGONI ambacho kinarushwa kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa nane mpaka saa kumi jioni

"Mimi kiukweli namkubali sana Rais Magufuli kwani hapo alipoanzia ni pazuri, hivyo sina tatizo kabisa na uongozi wa awamu ya tano, kuna kauli ambazo Mh. Rais Magufuli huwa anazitoa unaona kabisa ni mtu ambaye anathubutu kutenda, mfano hapindishi anasema kabisa ili tuweze kufanikiwa lazima tufanye kazi, hivyo sasa ni jukumu la serikali kuona inatengeneza namna nzuri hao vijana ili waweze kupata hizo ajira, watu wakapata huduma nzuri kulingana na kodi wanazolipa" alisema Rama Dee 

Rama alisisitiza kuwa kama kauli hizo za Rais Magufuli atazifanyia kazi na serikali ikatengeneza mifumo mizuri katika kila kitu basi anaamini nchi itasonga mbele.

"Kwa kuwa Rais ameonyesha huo uthubutu sasa ni jukumu la serikali kutenda kweli, hayo mambo ili tuweze kusonga mbele zaidi" alisisitiza Rama Dee