Breaking News

Waziri wa mazingira wa Burundi auawa

Waziri wa maji, mazingira na mpango wa ardhi wa Burundi Emmanuel Niyonkuru ameuawa kwa kupigwa risasi mapema leo majira ya saa 12:45 asubuhi alipokuwa njiani kurudi nyumbani kwake.

Msemaji wa polisi wa nchi hiyo Pierre Nkurikiye amesema hayo kupitia mtandao wake wa Twitter kuwa, waziri huyo amepigwa risasi akiwa anarudi nyumbani kwake eneo la Rohero.

Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza amesema hatua za kisheria zitachukuliwa kwa atakayepatikana na hatia ya mauaji hayo.