Obama amuonya Trump
Rais mwendazake Barack Obama amuonya Donald Trump kutoendesha shughuli za white House kama 'Shughuli ya biashara ya familia '.
Donald Trump atarajiwa kuanza shughuli zake rasmi kama rais wa Maekani mnamo Januari 20.
Obama alikuwa anaongea kupitia runinga ya Marekani ya ABC news na kutoa wito kwa Trump kuheshimu taasisi za Marekani.
Alisisitiza kuwa Trump anafaa kuwa mwanaglifu kwa hatua atakazo chukua
kwa kuwa atakuwa anaongoza kampuni kubwa zaidi duniani na nchi kubwa na
yenye nguvu zaidi duniani.
Obama alikuwa wazi kusema kuwa Trump alisababisha mashambulizi ya mitandaoni yaliyotekelezwa na Uruusi.
Aidha Obama alimpendekezea Trump kuwa na imani na mashirika ya ujasusi ya taifa.
Hapo awali Donald Trump amepinga mashirika ya kufanya uchunguzi ya Marekani.
Kremlin hadi leo imekataa kuhusika na udukuzi wa mitandao ya Marekani.
Hata hivyo mashirika ya habari ka CNN,Washington Post na NBC yametangaza
utambulisho wa majina ya watu waliohusika na udukuzi kutoka Urusi
wakati wa uchaguzi wa Marekani.


