Breaking News

Gabo Aahidi Kurejesha Heshima ya marehemu Kanumba....Tazama Video hapa Chini


Mshindi wa tuzo ya muigizaji bora wa kiume wa tuzo za EATV 2016, Salim Ahmed ‘Gabo Zigamba’ amefunguka kwa kuweka wazi mipango yake ya kazi ambayo itamfanya afanye mambo makubwa katika tasnia ya filamu kama aliyofanya marehemu Steven Kanumba.

Akiongea na Bongo5 wiki hii akiwa katika uzinduzi wa video mpya ya Belle 9, Gabo amedai tayari ameanza kuhudhuria workshop mbalimbali za maswala ya filamu ili kuangalia namna ambavyo anaweza kuipeperusha vizuri bendera ya Tanzania kimataifa.

“Ukiachana na mtazamo mdogo ambao watu wanautazama kuhusu tasnia ya filamu, ukiingia katika website yangu utaanza kuona jinsi ninavyojibrand, afanya bishara online, tayari kuna mawasiliano makubwa ya watu wa nje na ndani. Lakini kutumia nafasi hiyo hiyo tayari kuna mianya midogo midogo ambayo imenifanya nifanye workshop ndogo ndogo ambazo nimeanza kuhudhuria ili kuangalia wenzetu wanafanya vitu gani,” alisema Gabo.

Muigizaji huyo ambaye yupo chini ya Kampuni ya Vitamin Music Group Limited ya msanii wa muziki Belle 9, amedai mipango hiyo ni ishara tosha ambayo inaonyesha nini anaenda kukifanya katika miaka ijayo.