Breaking News

Balozi wa Urusi nchini Uturuki auawa



Balozi wa Russia nchini Uturuki Bw. Andrei Karlov ameuawa kwa kupigwa risasi mjini Ankara alipokuwa akihudhuria maonesho ya usanii.

Serikali ya Uturuki imemtaja mshambuliaji kuwa ni askari wa polisi.
Shambulizi hili limetokea siku moja kabla ya waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kwenda Moscow kwa ajili ya mazungumzo na wenzake wa Russia na Iran kuhusu suala la Syria.