Breaking News

Ndege ya Somalia yapata ajali wakati wa kutua kwenye uwanja wa ndege mjini Nairobi




Mamlaka ya viwanja vya ndege nchini Kenya KAA ilifunga kwa muda uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta JKIA baada ya ndege moja ya Somalia kupata ajali wakati wa kutua kwenye uwanja huo jana usiku.

Taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo imesema ajali hiyo imeathiri kuruka na kutua kwa ndege kwenye uwanja huo mjini Nairobi, lakini hakuna abiria aliyejeruhiwa katika ajali hiyo.

Maofisa wa mamlaka hiyo wamesema ndege moja kutoka Somalia ilitua kwa dharura kwenye uwanja huo na kwenda nje ya barabara.