Breaking News

MTOTO ATUNUKIWA "PHD" YA CHUO KIKUU CHA KILIMO SOKOINE

pichani ni mtoto akionyesha akionyesha tunzo ya shahada aliyopekea kwa niaba ya mama yake aliyefariki dunia miezi michache iliyopita

Novemba 25, 2016 Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo kilikuwa na sherehe ya mahafali ya 32 ya chuo hicho katika Kampasi ya Solomon Mahlangu “Nelson Mandela Freedom Square” Mazimbu mkoani Morogoro, kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu walihitimu masomo yao na kutunukiwa Shahada ya Awali, Shahada ya Umahiri na Shahada ya Uzamivu.

Katika hali ambayo iliyokuwa ni ya kuhuzunisha lakini pia ya kutia moyo, mtoto mmoja alipokea Shahada ya Uzamivu (PhD) kwa niaba ya mama yake aliyekuwa akisoma katika chuo hicho. Mama yake alifariki dunia kabla ya siku ya mahafali hivyo mtoto huyo akateuliwa kupokea shahada hiyo kwa niaba yake.