Rais wa Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo ,Joseph Kabila ni sharti aheshimu katiba na
kujiuzulu mwishoni mwa muhula wake ,waziri wa maswala ya kigeni nchini
Ufaransa Jean-Mark Ayrault amesema katika mahojiano na kituo cha habari
cha TV5.
Bwana Ayrault alikuwa akisisitiza wito aliotoa wiki iliopita wakati akiwahutubia wanafunzi mjini Paris.
Wakati
huu aliangazia madai kwamba Ufaransa imekuwa ikiingilia maswala ya
ndani ya DRC,akisema kuwa taifa lake haliko pekee kumkumbusha Kabila
kwamba lazima aheshimu sheria.
Aliambia kituo hicho:''Rais Kabila
lazima aonyeshe mfano .Ni lazima aheshimu katiba.Iwapo vikwazo
vitahitajika tutaamua kuvitekeleza.Nataka watu waelewe; Watu waliopo
katika mamlaka DRC ni lazima wawajibike.Iwapo wanahitaji amani nchini
mwao,iwapo wanajali hali ya watu wao ,ni lazima wafuate katiba''.
Ufaransa yatishia kuiwekea vikwazo DRC
Reviewed by Mipiko
on
12:35 AM
Rating: 5