Breaking News

Lulu Diva Aongelea Bifu Lake na Amber Lulu




Muuza sura kwenye video za Kibongo, Lulu Abass ‘Lulu Diva’ (pichani juu) na mwenzake Amber Lulu  hawana bifu lolote isipokuwa kuna watu wana mpango wa kuwagombanisha.

Akichonga na Risasi Vibes, Lulu Diva alifunguka kuwa awali aliposikia kuwa Amber alimpaka matope kwenye ‘interview’ aliyofanya na redio fulani Bongo, alipaniki na kumtafuta ili amueleze kulikoni, lakini Amber alimwambia hakuna kitu kama hicho na kumtaka kuchunguza mwenyewe.

“Nilichunguza na kukuta kumbe si kweli, niligundua ni watu wasiopenda ushoga wetu ndiyo walikuwa wanajaribu kutukosanisha na si vinginevyo,” alisema Lulu Diva.