Ludovic Utouh ashauri taasisi mbalimbali kujiunga na soko la hisa nchini
Uttoh ameyasema hayo Jijini Dar es salaam katika
utoaji Tuzo kwa taasisi mbalimbali zilizofanya vizuri kwenye ukuaji wa hisa zao
katika soko hilo Taasisi ambazo ni NMB,CRDB,MAENDELEO BANK,TBC,CITZEN na OBY
SECURITY.
UTOUH amesema ni vyema sasa Taasisi nyingine kuiga mfano huu ulionyeshwa na
taasisi nyingine nchini kujiunga na soko la hisa Tanzania.
“Soko hili lilianzishwa baada ya semina waliyofanya
Arusha ivyo ni soko change na makampuni yaliyopo katika soko hilo ni machache
hivyo ni vyema kwa Taasisi zetu kujiunga katika soko hili ili kujenga uchumi
bora kwa Taasisi nan chi kwa ujumla”ameeleza UTOUH.
Akizungumza katika hafla hiyo ya utoaji wa Tuzo
msajili wa hazina LAURENCE MAFURU amesema kuwa ili soko hilo la hisa liweze
kukua linapaswa kutambua na kushinikiza utawala bora Zaidi na pia kuna umuhimu
nwa kutoa elimu kwa taasisi mbalimbali ili kuweza kuelewa umuhimu wa soko hilo
nchini.
Aidha Mkurugenzi wa soko la hisa nchini Tanzania
MOREMI MARWA amesema kuwa wana mpango wa kushawishi taasisi nyingine nyingi
iweze kujiunga na soko hilo la hisa ili kukuza uchumi wa Taasisi hizo na Taifa
kwa ujumla ambapo amesema kuwa wanatarajia baada ya miaka 20 soko kukua Zaidi na
kuweza kujitanua katika maeneo mbalimbali


