Vita ya Panzi Furaha ya Kunguru Nchini Sudan Kusini
Wanasiasa pamoja na wakuu wa jeshi nchini Sudan Kusini wanaripotiwa
kujitajirisha wakati nchi hiyo inapoendelea kukumbwa na mapigano ya
wenyewe kwa wenyewe kulingana na ripoti ya shirika la Sentry
linalofadhiliwa na muigizaji George Clooney pamoja na mwanaharakati John
Prendergast.Waandishi wa ripoti hiyo yenye kichwa, Udhaifu wa Vita Haustahili Kujilipa, walisema kuwa walichunguza uhusiano uliopo kati ya wakuu nchini Sudan Kusini na pesa zilizonunua nyumba za kifahari na biashara nyingi za madini, mafuta na za kifedha.

Tofauti za wanasiasa waku wawili zilisababisha kutokea mapigano yaliyozuka mwezi Disemba mwaka 2013.
Ripoti moja ilisema kuwa , inaonekana watu wachache wanadhibiti asilimia kubwa ya uchumi wa Sudan Kusini na wengi wa watu hawa ni wale walio madarakani.


