Marekani imeadhimisha miaka 15 tangu shambulizi la kigaidi la 9/11 kwa njia tofauti kwenye sehemu mbalimbali nchini humo.
Akitoa hotuba kwenye bustani ya kumbukumbu ya tukio hilo iliyoko
wizara ya ulinzi, rais Barack Obama amesema tishio la ugaidi
linaloikabili Marekani kwa sasa limebadilika, kwa kuwa magaidi
wanajaribu kupanga mashambulizi madogo lakini yenye athari kubwa. Rais
Obama amesisitiza kuwa, watu wa tamaduni tofauti kuishi kwa pamoja ni
chanzo cha nguvu cha Marekani, na kuwataka wananchi washikamane na
kutoruhusu vitendo vyovyote vya kuleta mfarakano nchini humo.
Baadhi ya jamaa wa wahanga wa tukio hilo wameeleza kutoridhika na
sera ya sasa ya serikali katika kupambana na Ugaidi, wakiona nchi yao
iko hatarini zaidi kuliko wakati lilipotokea shambulizi la 9/11.
Marekani yaadhimisha miaka 15 tangu shambulizi la 9/11 litokee
Reviewed by Mipiko
on
9:42 AM
Rating: 5