Rais Dkt.Magufuli afanya ziara ya kushtukiza katika Shule ya Msingi Chato
Rais
Dkt Magufuli ameahidi kujenga madarasa matatu na ofisi moja ya walimu
katika Shule hiyo kufuatia ombi la Walimu kuwa shule hiyo inakabiliwa na
uhaba wa vyumba vya madarasa ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi
wanaosoma shuleni hapo.
Aidha
Dkt.Magufuli amewaasa wanafunzi kutilia mkazo masomo ili waweze
kufaulu na kuwataka walimu kuhakikisha wanatumia vyema fedha
zinazotolewa na Serikali kila mwezi katika kutoa elimu bila malipo
na pasiwe na wanafunzi hewa kama ilivyo kwa baadhi ya shule ambazo
zimegundulika kuwa na wanafunzi hewa katika uhakiki uliofanywa na
serikali.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia
pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Chato mkoani Geita. Shule hiyo ya
Msingi Chato ndiyo Rais Dkt. Magufuli alisoma kuanzia darasa la kwanza
mpaka Darasa la Saba. Rais Dkt. Magufuli amewaasa Wanafunzi hao kusoma
kwa bidii kwasababu yeye pia alisoma shuleni hapo.
|


