Breaking News

Zambia Yapata Pigo...yavamiwa na viwavi Hatarishi kwa Mazao




media
Miaka minne iliyoipita, viwavi waliteketeza mazao nchini Zambia.

Rais wa Zambia Edgar Lungu, ametoa wito kwa kikosi cha jeshi la anga kusaidia kukabiliana na uvamizi wa viwavi nchini humo. Zambia ilishuhudia tukio kama hilo miaka minne iliyopita.

Wadudu hawa wanateketeza mazao katika mikoa sita kati ya kumi inayounda nchi ya Zambia. Wadudu hao wana uwezo wa kuharibu mashamba yote.

Ndege za kijeshi zimeanza zoezi la kupulizia dawa za kuua wadudu katika maeneo yaliyoathirika zaidi.

Miaka minne iliyoipita, viwavi waliteketeza mazao nchini Zambia, hasa mahindi, mihogo, mtama na mchele.