
UNGA LISHE : Ni unga bora na unao
hitajika sana katika kuborehs afya za
watoto, wazee na wagonjwa. Ukiwa kama
mjasiriamali mdogo, ni muhimu kujua
namna ya kutengeneza unga lishe, kwani
malighafi zinazo tumika katika
utayarishaji wa unga huu zinapatikana
kwa wingi na kwa bei nafuu, hivyo basi
hata kwa wewe mwenye mtaji mdogo,
unaweza kufanya biashara hii bila ya
kuhitajika kuwa na mtaji mkubwa jambo
linalo chukuliwa kama changamoto kwa
wajasiriamali
wengi nchini.
MALIGHAFI ZINAZO HITAJIKA KATIKA
UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.
* Karanga - Nusu Kilo.
* Soya - Nusu Kilo.
* Ulezi - Kilo moja na Nusu.
* Mahindi -Nusu Kilo
*Mtama - Mtama Nusu Kilo.
* Uwele - Nusu kilo.
* Mchele - Nusu kilo..
JINSI YA KUTENGENEZA UNGA LISHE .
1. Safisha ulezi na kuutoa michanga
pamoja na vumbi.
2. Kaanga soya kwenye moto mpaka
ibadilike rangi na kuwa " brown " ama
kahawia.
3. Kaanga karanga zako na toa maganda.
Saga mchanganyiko wa malighafi zote
hapo juu kwa pamoja, kisha anika juani
mpaka ukauke, halafu weka kwenye
vifungashio kwa ajili ya kuuza.
MASOMO YA KESHO : Utengenezaji wa
Chilli Souce, Tomato Souce, Mango
Pickles, Keki, Soya Masalla, Wine Ya
Ndizi, Wine Ya Nanasi, Wine Ya Rossela,
Crips za Ndizi, Siagi Ya Karanga "
Peanut Butter ', Chaki, Kiwi & Mkaa Kwa
Kutumia Makaratasi na Vifuu vya Nazi.
ENDELEA KUTEMBELEA BLOGU HII, MARA
KWA MARA KWANI TUTAKUWA
TUKICHAPISHA MASOMO YA
UTENGENEZAJI WA BIDHAA ZOTE AMBAZO
TUMEZITANGAZA KATIKA MATANGAZO
YETU YA AWALI PAMOJA NA NYINGINE
ZA NYONGEZA AMBAZO HATUJA
ZITANGAZA.. KAMA UNA SWALI LOLOTE
LILE, MAONI, USHAURI AMA UNA BIDHAA YOYOTE AMBAYO UNGEPENDA TUIWEKE HAPA BLOGUNI TAFADHALI WASILIANA NASI KUPITIA MTANDAO WA WHATSAPP @0768548165