Breaking News

Wafuasi wa Prof. Lipumba wakamata magari ya CUF yaliyofichwa



prof-lipumba

Magari matano ya Chama cha Wananchi (CUF) yanayodaiwa kufichwa na baadhi ya wafuasi wa Katibu Mkuu wa chama hicho Maalim Seif Sheriff Hamad miezi kadhaa iliyopita yamepatikana maeneo ya Kimara-Bonyokwa jijini Dar es Salaam.

Mmoja kati ya walinzi wa CUF wa makao makuu ya ofisi za chama hicho, Jamal Yasin amedai kuwa magari hayo yamepatikana katika nyumba ya mfuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye hakumtaja jina na kwamba yanasafirishwa na kuletwa kwenye makao makuu ya ofisi za CUF yaliyopo Buguruni.

Yasin ameuambia mtandao huu kuwa, “Mchanjama alitoa taarifa ya sehemu iliyokuwepo magari kwamba ni maeneo ya Bonyokwa katika nyumba ya mfuasi wa Chadema jina lake halijajulikana, kundi la wanachama wanayarudisha ofisini Buguruni.”

Ametaja baadhi ya magari hayo kuwa ni Landcruiser na Toyota.